Sauti zote zinavyoimbwa pamoja na nota. Click hapa
MANENO
- Uje Roho Mtakatifu Tuangaze toka Mbingu, Roho zetu kwa mwangao.
- Uje Baba wa maskini Uje mtoa wa vipaji, Uje mwanga wa mioyo.
- Ee Mfariji mwema sana Ee rafiki mwanana, Ewe Raha mustarehe.
- Kwenye kazi u-pumziko kwenye joto Burudisho, Umfutaji wa machozi.
- Ewe mwanga wenye heri uwajaze waamini, Neema yako mioyoni.
- Bila nguvu yako wewe mwanadamu hana kitu, Kwake yote yana kosa.
- Osha machafuko yetu panyeshee pakavu petu, Na kuponya majeraha .
- Ulegeze ukaidi pasha moto ubaridi, Nyoosha upotovu wetu.
- Wape waamini wako wenye tumaini kwako, Paji zako zote saba.
- Wape tuzo ya fadhila wape mwisho bila ila, Wape heri ya milele.
- Amina Aleluya Amina Aleluya, Amina Aleluya.